
The Higher Education Student Loans Board (HESLB) today, Friday, October 24, 2025, has issued the first phase of loan planning and grants for a total of 135,240 students.
This number includes the following students:
- i. 40,952 undergraduate students and 5,342 diploma students were assigned loans amounting to TZS. 152 billion.
- ii. 615 Samia Scholarship students who were allocated a subsidy amounting to TZS. 3.3 billion.
- iii. 88,331 students who are continuing their studies have been allocated loans amounting to TZS. 271.2 billion after passing their exams of the previous year.
The Credit Board will continue to issue other installments of loans and scholarships as it receives confirmation of admission for first-year students and results for continuing students. In addition, the Credit Board reminds applicants for loans and grants to continue monitoring their application information through ‘SIPA’ while the analysis and planning procedures for loans and grants continue.
Recommended:
Issued by: Executive Director Higher Education Student Loans Board (HESLB) Friday, October 24, 2025
HESLB Majina ya waliopata Mkopo 2025/2026
Congulaturations you get the loan from HESLB For 2025/2026 Academic Year please visit the link below to check your allocation
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) leo Ijumaa, Oktoba 24,2025 imetoa awamu ya kwanza ya upangaji mikopo na ruzuku yenye jumla ya wanafunzi 135,240. Idadi hii inajumuisha wanafunzi wafuatato:
i. Wanafunzi 40,952 wa shahada ya awali na wanafunzi 5,342 wa stashahada waliopangiwa mikopo kiasi cha TZS. 152 bilioni.
ii. Wanafunzi 615 wa Samia Skolashipu waliopangiwa ruzuku kiasi cha TZS. 3.3 bilioni.
iii. Wanafunzi 88,331 wanaoendelea na masomo wamepangiwa mkopo kiasi cha TZS. 271.2 bilioni baada ya kufaulu mitihani yao ya mwaka uliotangulia.
Bodi ya Mikopo itaendelea kutoa awamu zingine za mikopo na skolashipu kadiri itakavyopokea uthibitisho wa udahili kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza na matokeo kwa wanafunzi wanaoendelea na masomo.
Read Also:
Aidha, Bodi ya Mikopo inawakumbusha waombaji wa mikopo na ruzuku kuendelea kufuatilia taarifa za maombi yao kupitia ‘SIPA’ wakati taratibu za uchambuzi na upangaji wa mikopo na ruzuku zikiendelea.
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mtendaji
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB)
Ijumaa, Oktoba 24, 2025
| Hatua | Maelezo ya Kufanya |
|---|---|
| 1. Fungua Tovuti Rasmi ya HESLB | Nenda kwenye tovuti ya https://olas.heslb.go.tz kupitia simu au kompyuta yenye intaneti. |
| 2. Bonyeza “Login to OLAMS” | Ukifika kwenye ukurasa wa mwanzo, chagua sehemu ya “Login to OLAMS” au “SIPA Account” kwa waombaji wa mkopo. |
| 3. Ingiza Taarifa Zako za Kuingia | Andika Email au Namba ya Maombi (Form Four Index Number) pamoja na Neno la Siri (Password) ulilounda wakati wa kujisajili. |
| 4. Fungua Dashibodi Yako | Baada ya kuingia, utaona dashibodi yako ya OLAMS yenye taarifa zako binafsi na za mkopo. |
| 5. Bonyeza Sehemu ya “Loan Status” | Chagua kipengele cha “Loan Status” au “Allocation Results” ili kuona kama umepewa mkopo na kiasi kilichotolewa. |
| 6. Pakua au Chapisha Taarifa | Unaweza kupakua (Download) au kuchapisha (Print) taarifa ya mkopo kwa matumizi yako ya baadaye. |
| 7. Kagua Mara kwa Mara | Ikiwa majibu yako hayajatoka, endelea kuangalia mara kwa mara kwani HESLB huendelea kusasisha orodha kwa awamu tofauti. |